Mbunge wa Singida Mashariki na Rais wa Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS), ambaye kwa sasa yupo nje kwa dhamana dhidi ya kosa la uchochezi, amefunguka jinsi maaskari walivyomkamata na kutaka kupima haja ndogo bila sababu maalumu.
Mhe Lissu amesema niliwakatalia kwa sababu nilishitakiwa kwa kosa la uchochezi na sio kosa lingine na kama wangemshitaki kwa kosa lingine linalomtaka afanye hivyo basi kisheria angefanya hivyo.
“Mimi nimeshtakiwa kwa uchochezi kupima mkojo, unadhibitishaje uchochezi na kupima mkojo? wakaniambia kuna vitu wanavitafuta, mimi nikawambia mkanishtaki na vitu hivyo kwanza ili muende kwa hakimu mkapate order ili mje mchukue mkojo wangu… anyway mimi niliwakatalia”,amesema Tundu Lissu kwenye mkutano wake na waandishi wa habari mapema leo baada ya kuachiwa kwa dhamana.
Hata hivyo Mhe Lissu amesema asingekubali kupima mkojo kwani kufanya hivyo angebambikiziwa kesi na kutengeneza headline kwenye magazeti.
No comments