Followers

Theme images by tomograf. Powered by Blogger.

ENTERTAINMENT

GOSSIP

INTERNATIONAL NEWS

LOCAL NEWS

» » POLISI WAFANYA UPEKUZI TENA NYUMBANI KWA ASKOFU GWAJIMA.


Wakili  wa Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na uzima, Askofu Josephati Gwajima,  Peter Kibatala amesema kuwa polisi wamefanya upekuzi kwa mara nyingine nyumbani kwa Askofu huyo.
Kibatala ambaye ni wakili wa Askofu Gwajima amesema kuwa mbali na kupekuwa nakupiga picha kila kona ya nyumba pia walikwenda katika kanisa lake lililopo Ubungo kwa ajili ya upekuzi.
“Waache wafanye yao na sisi tutafanya yetu kisheria, Kwani hatuwezi kuwazuia Polisi kufanya shughuli yao na baada ya kumaliza na sisi tutajua nini cha kufanya,” amesema Kibatala.
Msemaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, David Mngongolwa amesema Gwajima alikwenda polisi kuripoti kama alivyoamriwa kufanya hivyo.
Aidha, Mngongolwa ameongeza kuwa baada ya kuripoti askari walimchukua na kwenda naye nyumbani kwake kwa ajili ya upekuzi na baada ya hapo waliondoka naye.
Hata hivyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Suzan Kaganda amesema hana taarifa za kukamatwa kwa Gwajima kwa maelezo kuwa alikuwa katika kikao.
source DAR24
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

About the Author Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

No comments

Leave a Reply

MOVIE

VIDEO

FASHION

Cat-5

MUSIC