Followers

Theme images by tomograf. Powered by Blogger.

ENTERTAINMENT

GOSSIP

INTERNATIONAL NEWS

LOCAL NEWS

» » GAMBIA : WANASHERIA WAUNGANA KUSHINIKIZA RAIS YAHYA JAMMEH KUKABIDHI MADARAKA


Muungano wa wanasheria nchini Gambia umesema kuwa kitendo cha Rais wa nchi hiyo Yahya Jammeh kukataa matokeo ya kura zilizoonyesha kuwa ameshindwa katika uchaguzi uliopita ni kuisaliti nchi hiyo.

Muungano huo umeitisha maandamano kwa nchi nzima mpaka pale Jammeh aliyeangushwa katika uchaguzi huo akabidhi madaraka.

Hapo awali Jammeh alikubali kushindwa na kuahidi kuondoka madarakani lakini aliyakataa matokeo hayo siku ya Ijumaa.

Ujumbe wa wakuu wa nchi za Afrika unatarajiwa kusafiri kuelekea Gambia siku ya Jumanne kwa lengo la kuzungumza na Jammeh ili kuachia madaraka.

Marekani imeonya kuwa nchi hiyo inapitia katika mazingira magumu huku baadhi ya viongozi wa kijeshi wakitajwa kumuunga mkono Jammeh.

Ujumbe wa wakuu wa nchi za Afrika unatarajiwa kuwajumuisha Rais wa Nigeria, Ghana, Liberia na Siera Leone.

Kwa upande wake Baraza la usalama la umoja wa mataifa linajadili namna ya kutatua mgogoro huo leo.

SOURCE BBC SWAHILI
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

About the Author Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

No comments

Leave a Reply

MOVIE

VIDEO

FASHION

Cat-5

MUSIC